Skip to main content

THE HUNTER

 CHAPTER TWO.



Miaka kumi baada ya tukio.

Kijana mmoja anashuka kwenye ndege kwenye uwanja wa ndege wa mwalimu Nyerere huku akivaa nguo nzuri za gharama na kupokelewa na mwanaume mwingine aliyekuwa anamsubiri.

   "habari yako bosi pole kwa safari" alisema yule mtu aliyekuwa anamsubiria

  "salama James za siku nyingi?" aliuliza yule bosi kwa sauti yake ya kukwaruzakwaruza kama mtu aliyekabwa hali hiyo ilimuuma ila hakuwa na jinsi na ameshaanza kuzoea

    "salama mkuu" alisema James

    "Twende zetu home tutajua la kufanya"alisema bossi

    "sawa bosi"alisema huku akitaka kuchukua mizigo ila alikuta bossi kashaichukua na kuiweka kwenye buti ya gari

    "sasa bosi si uache nikusaidie" alisema James

    "unisaidie..... KWANI UMESIKIA MIMI NI MLEMAVU?" aliuliza bossi kwa jazba

   "hapana mkuu"alijibu Jamesi kwa hofu

   "Dah!! saamahani bhana alisema bossi huku akiachia ule mzigo aliokuwa nao ili James aubebe, hali hiyo ilamshangaza sana James maana alikuwa anajua kuwa mkuu wake ni mkorofi pia alihisi ni mtu mwenye hasira muda wote ila alichoambiwa na ukweli wenyewe ni vitu viwili tofauti.Wakapanda gari na kuanza safari ya kwenda Kilimanjaro.

            Mjini Moshi kwenye jengo la kilimani ofisi za kampuni kubwa ndani ya ofisi kuna mwanaume mwenye umri wa miaka 30 akiwa ameweka miguu juu ya meza na mbele ya meza kuna utambulisho wa jina lake ambalo ni David ambaye ni mtoto wa bwana Jacson Urasa ambaye alifariki na kumuachia hizo mali ambazo zilisimamiwa na mama wa kambo aliyeitwa mama James.

       " habari yako mwanangu" ilisikika sauti ya mwanamke ikimsalimia David naye alikuwa ni mama James

       "salama shkamoo mama" alijibu David

       "marhabaa umeshndaje?" aliuliza mama James

      " salama sijui wewe mama?" aliuliza David

       "mimi niko salama nimepata habari kutoka kwa James kwamba yule mgeni anakuja sasa tujiandae" alisema mama James

      "sawa mama anakuja saa ngapi?" David aliuliza

      "atafika jion nahisi atakuwa hotelini labda kindoroko ila sijajua hivyo fanya ukampokee sawa?" alisema mama James

      "sawa mama kwani si tuende wote?" aliuliza David

      "mh!! ila nina kazi nyingi sana" alisema Mama James

      "mh! mama kazi haziishagi twende wote" alisema David

      "tangu uache bodaboda umekuwa mstaarabu sana" alisema mama James "okay sawa tutaenda wote na usiendeshe gari kama kichaa" aliongezea

            Upande wa bossi na James walikuwa safarini kuelekaea Kilimanjaro huku James akiwa na furaha sana ila Bossi wake akiwa na wasiwasi.

         "Bossi mbona unawasiwasi?" aliuliza James

        "nawaza James alafu usiniite Bossi" alisema Bossi

       "sasa unataka nikuiteje nikuite jina lako ili kilamtu akujue au nikuite hivihivi?" aliuliza James

       "Haya bhana ila twende kufuata mpango wetu au unasemaje? aliuliza Bossi

       "ndoivo tunavyotakiwa"alijibu James huku akitabasamu

        "ila bosi nilitakiwa nikuite wewe" alisema Bossi

         "acha ujinga wewe unastahili hili jina kwahiyo sitaki kuusikia huvyo na wewe unajua kwanini unaitwa hivyo"alisema James

     "kwani nimekataa?" alisema Bossi nayo safari ikayoyoma walipokaribia moshi walipiga simu nyumbani ili kuwapa taarifa ya safari yao

     "Halo shkamoo mama" alisema James kumsalimia mamaye

     "marhaba mwanangu hujambo?" aliuliza mama James

     " sijambo sisi ndo tumefika kiborloni" alisema James

     "Sawa" alisema James kisha akakata simu

    "Haya tutawakuta kwanye kituo cha mabasi cha moshi mjini" alisema James kumwelekea Bossi wake

    " ok sawa" bossi alijibu huku akipiga muayo

            Huku nyumbani kwa mama Jamesi akiwa anajiandaa akampigia simu David ajiandae kumpokea huyo mgeni atakayekuja ambaye hata wao hawamjui kwa sura na ni mgeni muhimu katika kampuni ambapo wanamsubiria ili kuisaidia kampuni dhidi ya kufilisika.Baada ya David kufika tu walipanda gari na kuanza safari yao kuelekea kituo cha mabasi Moshi mjini walipofika walishuka na kumsubiri mgeni wao kwenye kiamgahawa ka fresh coach. Mji ulikuwa na baridi kiasi ambayo ilifanya mji kupoa na pia kelele za watu kama nyuki kwenye mzinga zilifanya mji uendelee kupendeza ila hali ilibadilika baada ya James kufika na mgeni wake papo hapo hali joto iliongezeka na dunia yote ikakaa kimya kanakwamba walipata uziwi wa ghafla nao muda ulisimama ukawa unawnda taratibu sana hawakuamini kilichoendelea.

      "ha...ha...haiwezekani" alisema David

     " nini eh!! mbona un...." mama James hakuweza kumalizia baada ya kumwona Bossi hali yake ikabailika na kuanza kutapatapa kama samaki nje ya maji asijue la kuongea huku akimhisi David kuwa amepanga njama za kumuharibia na kumpindua ila haikuwa hivyo maana hata yeye alikuwa na hofu ya kutosha

Comments

Popular posts from this blog

THE UNKNOWN

  CHAPTER SIX Previously Detective’s daughter was kidnapped by a stranger then a man ran to the police station with blood all over him and said he didn't want to die so what happened next…….. Continue…. “Please put me in jail” a blooded man said “Why?”  a confused police asked            "Am the one who kidnap detective's daughter" a blooded man said             "So where is the child?" A police asked               "In my safe house" he answered            "So can you go with us?" A police asked            '' i can't she is hunting me"  the blooded man said with frightened voice             "Ok calm down you'll be with ...

THE UNKNOWN

     CHAPTER FIVE                                   Previously on chapter four  A detective's house was stalked by an unknown man so he starts and also the killer knows every move that he takes so what should he do?    Continue.       That event sent butterflies to his stomach and he was deathly scared about her family's safety. He asked himself what to do next and how he would save his family.         "Good morning dad" said Rehema         " Good morning how was your night dad" he asked while forcing smile on his face           "Was super great when your here with us" she answered while smiling          "Good morning baba Rehema" his wife greeting...

THE UNKNOWN

CHAPTER FOUR   Previous on chapter three. Some suspicious appear in between the team because of the new detective, while new murder take place. Continue.      Since the first murder there's no any news media which report about the case so the detective Patrick take a little break because he didn't stand on his house's door for weeks now and his family didn't see him for about a month or so. So he carry three bags with him to his family.    " Hodiii" he knock the door.    "Karibuuu" a female voice answered as she run to open the door     "Asante" he answered     " Shikamoo Baba" a female voice greet   "Marahaba my daughter how are you?" He asked after answered     "Am fine how are you?" She asked     " Am fine my daughter " he answered    "Mama dad is here" she said loud to her mother and then she said"dad did you know I have...